Batarokota kulirudisha kundi la G tha Dunia


Pichani juu kushoto Batarokota akiwa na Cide Boy 

MKALI wa rapu nchini Tanzania ambaye ni mkurugenzi wa Batarokota Social Media, Paskal Linda a.k.a Batarokota, amedai anataka kulirudisha kundi hilo na kufanya shoo ya pamoja kwa ajili ya kumkumbuka nyota wa muziki huo, Notorious B.I.G. ambaye alifariki 1997.


Shoo hiyo inatarajiwa kufanyika Mei 21 ukumbi wa Brooklyn 44 Nairobi nchini Kenya, siku ambayo B.I.G alizaliwa, ambapo angetimiza miaka 44.


Mara ya mwisho kundi la G tha Dunia kufanya onyesho la pamoja ilikuwa mwaka 2002 kwenye Toure ya Tabora nchini Tanzania.“Hii itakuwa shoo ya kihistoria katika historia ya muziki wa hip hop ambapo wasanii wenye majina Bid d, Ngollo 2, Dj Zari wamealikwa,” alisema Batarokota.

Neyo, Diamondi, Batarokota kutumbuiza Jembeka Festival 2016!


Siku ya kumbukumbu ya kukumbuka ajali ya MV Bukoba tareehe 21/05/2016 katika jijini la mawe Mwanza (Rocky City)  kutakuwa na burudani kabambe sana itakayo wakutanisha wasanii wengi wa ndani na nje ya Tanzania kama Neyo, Diamond, Batarokota na wasanii wengine kibao katika show inayotambulika kama Jembeka Festival 2016 chini ya udhamini wa JEMBEKA na VODACOM show ihi iliyopangwa kufanyika katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

MICHANO: DAZ BABA NAYE ANAHITAJI MSAADA KAMA CHID BENZI

YAP...yap...yap...Michano leo inamchana Daz Baba mwanaharakati aliyetumbukia kwenye shimo la madawa ya kulevya, kiukweli amepoteza mwelekeo ingawa kazi ni kazi ila inasikitisha pale anapoendesha maisha yake kwakupiga debe kwenye vituo vya daladala.
Huyu jamaa alikuwa kiongozi wa kundi kubwa na maarufu la muziki wa kizazi kipya la Daz Nundaz lenye maskani yake Sinza Dar es Salaam, kundi hilo lilijumuhisha wasanii watano akiwemo yeye.
Ila kwa sasa kundi hilo halipo tena yaani kwa maana nyingine limekufa, Daz Nundaz lilijipatia unaarufu mkubwa hasa kwa kuimba nyimbo za huzuni kama Kamanda, Maji ya shingo, Barua na nyinginezo nyingi.
Aidha Daz Baba binafsi amepata kutamba na nyimbo zake kama Elimu dunia, Umbo namba 8, Wife, Nipe tano na nyingine, kwa sasa jamaa anahitaji msaada wa kutupiwa kamba ili aishike na atoke kwenye shimo la madawa ya kulevya.
Kama mmeweza kumpa kamba Chid Benz basi kamba hiyo mpeni na Daz Baba kiongozi wa zamani wa kundi la Daz Nundaz lililojumuhisha vichwa kama Ferooz Mrisho, Sajo, Larhumba, Critic na Daz mwenyewe.
Hata hivyo inaonyesha tabia ya kuiga na kukata tamaa ndio chanzo cha matumizi ya madawa ya kulevya, Michano inamshauri Daz Baba anapochoma kuni asishangae majivu.
Tukutane Wiki ijayo kwenye Michano inayojenga na si kubomoa inayotayarishwa na Rapa Mkola Man mwenye chimbo lake Hale jijini Tanga, Ciao

Hongera Dk. Shein, lakini Zanzibar inahitaji umoja.


Katuni.
Juzi Zanzibar ilifanya uchaguzi wa marudio wa Rais, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani, ambao ulimpa ushindi wa asilimia 91.4 mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Ali Mohamed Shein.
 
Uchaguzi huo ulifanyika kutokana na matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana kufutwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec), Jecha Salim Jecha, kwa madai kuwa ulijaa kasoro kadhaa.
 
Hata hivyo, uamuzi wa Jecha ulikosolewa na makundi kadhaa wakiwamo waangalizi wa kimataifa wakisema katika ripoti yao ya awali kuwa ulikuwa mzuri kuliko hata wa mwaka 2010.
 
Chama cha wananchi (CUF) ambacho ni chama kikuu cha upinzani Zanzibar kilipinga maamuzi ya Jecha na kutangaza kutoshiriki katika uchaguzi wa marudio kwa kuwa kinatambua uchaguzi halali ni uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana.
 

Full Movie With English Subtitles - Tom And Jerry ...

Yanga wajipange kufuta uteja Al Ahly


Katuni.
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanznia Bara, timu ya Yanga wamefanikiwa kutinga raundi ya pili ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika baada ya juzi kuing'oa klabu ya APR ya Rwanda kwa jumla ya mabao 3-2.
Wanajangwani walishinda 2-1 ugenini jijini Kigali wiki mbili zilizopita kabla ya juzi kulazimishwa sare ya 1-1 nyumbani dhidi ya timu hiyo ya Jeshi la Rwanda.
 
Kabla ya kuivaa APR, Yanga iliikabili Cercle de Joachim ya Mauritius na kuitua nje ya michuano hiyo mikubwa zaidi kwa ngazi ya klabu barani kwa jumla ya mabao 3-0.
 
Kwa kutinga raundi ya pili, Yanga sasa itakuwa na kazi ngumu itakapochuana na Al Ahly ya Misri kwa mara nyingine baada ya msimu mmoja.
Timu hiyo ya Ligi Kuu ya Misri iliing'oa Yanga katika michuano ya Afrika mwaka juzi katika hatua ya matuta baada ya kutoka sare ya 1-1 katika muda wa kawaida, kila timu ikishinda nyumbani.
 
Takwimu za soka zinaonyesha timu za Tanzania zimekuwa zikitolewa mara nyingi kwenye michuano ya Afrika na timu za kaskazini mwa Afrika (za Kiarabu). Kutokana na ukweli huo, Nipashe tunaona kuna haja Yanga kufanya maandalizi ya kina kabla ya kuwavaa Al Ahly.
 
Timu za Kiarabu zinasifika kwa kuwa na mipango mizuri ya nje na ndani ya uwanja katika kusaka matokeo. Yanga wanapaswa kujipanga kikamilifu kuhakikisha wanadhibiti mianya ya fitna za Al Ahly.
 
Na kama kweli wamedhamiria kulipa kisasi cha matokeo mabaya ya mwaka juzi, tunafikikri Yanga wanapaswa kuanza maandalizi mapema kabla ya kukutana nao.
 
Licha ya kufanya vizuri katika raundi mbili zilizopita, tunaamini kikosi cha Yanga kinakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zisizofanyiwa kazi mapema, zitakuwa na athari kubwa mbele ya nyota wa Al Ahly wasiofanya makosa mengi wanapokuwa na nafasi ya kuifunga timu pinzani.
 
Katika mechi mbili zilizopita dhidi ya APR, kwa mfano, Yanga imeruhusu mabao mawili na safu zake zote kuanzia ulinzi hadi ushambuliaji zilionekana kuyumba.
 
Tunafahamu kuna changamoto ya kuwa na majeruhi kadhaa kikosini, lakini Yanga ilisajili nyota 24 kwa ajili ya msimu huu ambao tunaamini wakielezwa mbinu chafu na fitna za timu za Kiarabu, wanaweza kutinga robo-fainali kwa kuing'oa Al Ahly na kuiwakilisha vyema Tanzania msimu huu.
 
Al Ahly iliyoanzishwa Aprili 24, 1907 (miaka 28 kabla ya Yanga kuanzishwa), ina rekodi nzuri katika mashindano ya Afrika, Timu hiyo imeshinda mataji nane ya Ligi ya Mabingwa na moja la michuano ya Kombe la Shirikisho.
 
Tunafahamu pia kuwa Al-Ahly ndiyo timu namba moja duniani kwa kushinda mataji mengi ya kimataifa (Klabu Bingwa duniani) wakifanya hivyo mara 20 na kuzipiku AC Milan, Real Madrid na Boca Juniors.
 
Lakini mpira unadunda, Yanga walikaribia kuing'oa mwaka juzi, tunaamini wanaweza kupata mafanikio hayo mwaka huu.
 
Ndiyo maana tunatoa rai kwa uongozi wa Yanga na benchi lao la ufundi kujipanga vyema ili kupata matokeo mazuri nje-ndani dhidi ya timu hiyo
 
SOURCE: NIPASHE

Kwa aina hii ya maandalizi, medali Olimpiki ndoto

 TANZANIA inajiandaa kushiriki michuano ya kimataifa ya Olimpiki itakayofanyika Agosti mwaka huu  nchini Brazil.
Michuno hii mikubwa ya kimataifa, hufanyika mara moja kila baada ya miaka minne na kushirikisha mataifa mbalimbali duniani.
Zaidi ya michezo 50, ukiwamo soka hushindaniwa kwenye mashindano haya ya pekee na aina yake.
Tanzania ni moja ya nchi zinazotarajia kupeleka wawakilishi watakaoshindana katika michezo hiyo.
Ingawa kuna michezo zaidi ya 50 inayoshindaniwa, Tanzania itapeleka wawakilishi katika michezo mitatu; Judo, riadha na kuogelea.
Hata hivyo, pamoja na Tanzania kutuma wawakilishi kwenye mashindano haya kila yanapofanyika, bado hakuna mafanikio ya kujivunia.
Sababu kubwa ambayo imekuwa kama wimbo kwa Tanzania kushindwa  kupata mafanikio ni maandalizi duni.
Maandalizi ya zima moto kwa wanamichezo wetu katika mashindano mbalimbali, ndiyo kiini cha kushindwa kufanikiwa.
Kwa wenzetu wanaopenda mafanikio na ndiyo ambao leo wanaendelea kufanya makubwa katika mashindano ya kimataifa, hujiandaa mara tu mashindano ya awali yanapomalizika.
Hawana muda wa kusubiri hadi mashindano yanapokaribia ndipo waanze maandalizi kama tunavyofanya sisi.
Katika hali ya maandalizi ya aina hii, hatuwezi kupata mafanikio. Pengine sifa kubwa itakuwa ni ushiriki  usio na tija.

Mchora vibonzo 'Gado' kumshtaki muajiri wake

Mchoraji vibonzo wa Kenya Godfrey Mwapembwa ,aka Gado ameiambia BBC kwamba atalishtaki gazeti la The daily Nation nchini Kenya kuhusu kile alichokitaja kuwa kusimamishwa kwa kandarasi yake kinyume cha sheria.

Azam, Yanga kazi haijaisha Afrika.


Katuni.
Mwishoni mwa wiki timu za Azam na Yanga zilifanya vizuri katika mechi za kimataifa ugenini huku JKU ya Ligi Kuu ya Zanzibar ikikumbana na kipigo jijini Kampala, Uganda.
 
Yanga iliyokuwa ugenini kwenye Uwanja wa Amahoro jijini Kigali, Rwanda, iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji APR FC katika mechi ya kwanza ya Raundi ya Kwanza ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika.
 
Azam FC walichomoza na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Bidvest Wits mjini Johannesbrug, Afrika Kusini katika mechi yao ya kwanza ya Raundi ya Kwanza ya Kombe la Shirikisho.
 
Wawakilishi pekee wa Zanzibar waliosalia kwenye michuano ya Afrika mwaka huu, JKU FC wakitandikwa magoli 4-0 dhidi ya SC Villa ya Ligi Kuu ya Uganda na kufifisha ndoto zao za kutinga Raundi ya Pili ya michuano ya Kombe la Shirikisho.

Coming Soon!